Thursday 17 January 2013

Umangati wengia kidedeani!!!

Mzee nimebaini, wana wanaofanana,
Hawatiki tofutini, wana mfanano wana,
Hawaji tena mjini, maswala kuchanjiana,
Umangati nauona, wangia kidedeani.

Acha nikwelezeni, hali zino mzelewe,
Umangati huno nini, na kidedea mjuwe,
Kinipata makosani, niteteni nisiwawe,
Umangati nauona, wangia kidedeani.

Nakumbuka utotoni, nilipokuwa na meno,
Nikiwa kwetu nyumbani, kwa baba na mama Chano,
Nikifundwa ya ujani, nilona haya maono,
Umangati nauona, wangia kidedeani.

Nilifundwa umangati, na mama pia na aba,
Si wema niwe sifwati, katika la siku saba,
Kwani huakupi cheti, kichora itesha raba,
Umangati nauona, wangia kidedeani.

Umangati huahidi, ahadi zilo kamili,
Huapisha ikibidi, ja wa Kwale Mswahili,
Lakini ngoma kurudi, ahadi kuitimili,

Umangati nauona, wangia kidedeani.
Kisha kuna kidedea, nifundishwa na wavyele,
Hiki cheza kuelea, na hurowa kwa utele,
Walinomba kwendelea, kizingatia milele,
Umangati nauona, wangia kidedeani.

Eti kina kumanisha, wazaaji walinena,
Halafu nisha wazisha, wankwisha ozeana,
Leo nona cha kutisha, kidea kina mikuna,
Umangati nauona, wangia kidedeani.

Ino mikuna naona, ni ile ya kimangati,
Ndo mana wazi nanena, kimengia umangati,
Vipi ikawezekana, kushangaa miye sati,
Umangati nauona, wangia kidedeani!!


Siddi Kiroboto Mpole
Mzee Kimpole”
Kimpola Language School,
Eldoret.