Toloi kupata wana
Mpole ninaingia, na hongera
chekwachekwa,
Nampongeza Rukia, Waluhya tunamjuwa,
Mola amemjibia, kwani wana amepewa,
Toloi kupata wana, ni ishara yake
Mungu.
Ni ishara yake Mungu, Bwana wa wokovu
wetu,
Tumpe yetu machungu, anaweza vyote
vitu,
Mwenye dunia na mbingu, alomkumbuka
Lutu,
Toloi kupata wana, kuimarishe imani.
Kuimarishe imani, kati yetu waumini,
Tutambue Mungu nani, tudumu kumuamini,
Siyumbeyumbe jamani, wala simjaribuni,
Toloi kupata wana, kweli ni mwamko
mpya.
Kweli ni mwamko mpya, tulioupata waja,
Liwe ni fundisho Kenya, kuwa maombi
daraja,
Bwana Mungu wa Eliya, tatupa
tukimngoja,
Toloi kupata wana, ni furaha kwetu
sote.
Ni furaha kwetu sote, tunamtukuza Mola,
Mungu Muweza wa yote, asante kujibu
sala,
Tuzuie tusikwate, wewe huna kibadala,
Toloi kupata wana, ni hidaya kubwa
hino,
Ni hidaya kubwa hino, Kiroboto
naswifia,
Namwinua Mungu mno, tena namsujudia,
Katimizia maono, wale nilohurumia,
Toloi kupata wana, la ziada sina tena.
La ziada sina tena, ila nasaha hatima,
Toloi leeni wana, kwa ndia iliyo njema,
Wakamheshimu Bwana, isiwapate nakama,
Toloi kupata wana, shangwe Mulembe Ef
Emu.
Ochieng’ O. Sylvester
“Kiroboto Mpole”
Chuo Kikuu Cha Moi
Chepkoilel.
Kwaheri Mrono
Mpole nina kilio, kilio cha Kiswahili,
Silipati kimbilio, kulitia pigo hi9li,
Mauti faradhi ndio, bali hiki kikatili,
Kwaheri ndugu Mrono, mwalimu wa heba
kubwa.
Twamshukuru Rabuka, kwa maishayo
mwandani,
Sie tutakukumbuka, kwa kaziyo vitabuni,
Kukupeza ni hakika, sautiyo redioni,
Kwaheri ndugu Mrono, mwalimu wa heba
kubwa.
Wapenzi wa Kiswahili, tumebaki vinywa
wazi,
Kote metulia tuli, tangu lizame jahazi,
Mwenzetu kwa kwenda mbali, umetutia
duwazi,
Kwaheri ndugu Mrono, mwalimu wa heba
kubwa.
Bahari yetu si shwari, imechafuka
watani,
Tangu uwe mhajiri, hatwoni chako
kifani,
Twafazaika twakiri, hatutaki kuamini,
Kwaheri ndugu Mrono, mwalimu wa heba
kubwa.
Kaketu wende salama, mikono yetu
twapunga,
Wasalimie wa zama, akina Mwalimu Mbega,
Twakwombea kwa Karima, na dhiki
atakutenga,
Kwaheri ndugu Mrono, mwalimu wa heba
kubwa.
Kituoni nikifika, rambirambi nazituma,
Makiwa ndu’ watukuka, nayo familia
nzima,
Haya mambo ya Rabuka, nayo mauko
lazima,
Kwaheri ndugu Mrono, mwalimu wa heba
kubwa.
Ochieng’ O. Sylvester
“Kiroboto Mpole”
Chuo Kikuu Cha Moi
Chepkoilel.