Eddi nipelo sikizi, Mpole
nasema nawe,
Umegeuka kilizi, sababu
nomba nijuwe,
Una nini siku hizi,
tuambie tukijuwe,
Wanga wawa dume gani,
kulialia ja mwana.
Kulialia ja mwana, redioni
gazetini,
Kifo nani hataona, ndo
kijaze mdomoni,
Unawapotosha wana, toa
mfano mwanani,
Wanga wawa dume gani,
Mpole nakushangaa.
Mpole nakushangaa, malenga
wa Visramu,
Kijua umekomaa, kumbe bado
kuhitimu,
Ni bora ukinyamaa,
usidhaniwe wazimu,
Wanga wawa dume gani,
nahurumia mkeo.
Nahurumia mkeo, kwani
kulea hakomi,
Hamna aso upeo, acha
kuzitoa kemi,
Hujui kifo ni cheo, sio
cha mapeni kumi,
Wanga wawa dume gani,
wawasiwasika bure.
Wawasiwasika bure, hakuna
anokwandama,
Zikumbuke hamrere, kwa
wengi ulizotuma,
Ndizo zafanya uhare, pole
hutaki kusema,
Wanga wawa dume gani,
wanishangaza Mpole,
Wanishangaza Mpole, mie
mkongwe bondeni,
Wazileta siku zile, Kizere
kivuma ndani,
Uje kwangu tuselele, juma
zima mafunzoni,
Wanga wawa dume gani,
kulia achia wana.
No comments:
Post a Comment