Mzee ni ukumbini, na tabu
la ujanani,
Natia macho miwani,
nimsomee Fulani,
Maisha ya duniani, wangi
hawajui nini,
Chombo kikitia nanga, si
mwisho wa usafiri.
Si mwisho wa usafiri, hata
kama umefika,
Huishi kwenye bandari,
kwenda zaidi tataka,
Ipe mgongo bahari, na
uikabili njia,
Chombo kikitia nanga,
teremka kwa makini.
Teremka kwa makini,
uikague sehemu,
Jua lengo kuu nini, nakili
kwa tarakimu,
Kama ndipo ubaini, lau
sipo ufahamu,
Chombo kikitia nanga,
yasubiri maelezo.
Yasubiri maelezo, usanze
bure kuranda,
Yako kote matatizo, kokote
unakokwenda,
Hayakeri maulizo, wangi
mno mewalinda,
Chombo kikitia nanga,
usanze kutoa mali.
Usanze kutoa mali,
itatwaliwa haraka,
Ufikiri mara mbili,
uhakiki umefika,
Wanolipuuza hili, huchekwa
wanapotoka,
Chombo kkitia nanga,
sikiza yao wazee.
Sikiza yao wazee, kama
miye Kimpole,
Tukiteswa tutetee, radhi
tulinazo tele,
Acha nende waombee, Mola
awone milele,
Chombo kikitia nanga,
umkumbuke Rabuka.
No comments:
Post a Comment