Mbogholi
ni
malaika?!
Mkwiro
naukamata, kigoma nanzekipiga,
Mati
natakaziita,
zone
Mbogoli
kikoga,
Huyu
mtoka Taveta, uungu akauiga,
Mbogholi
ni
Malaika,
waja
awona
shetani.
Waja
awona
shetani,
hasa
wale
wa
siasa,
Amewatia
doani,
eti
ni
hakimu
sasa,
Natakajua
ni nani, Ludo amemtakasa,
Mbogholi
ni
Malaika,
adharau
viongozi.
Adharau
viongozi, akawaita mikia,
Eti
kikaza
maozi,
awaona
masinia,
Naona
akosa
kazi,
wengine
kawangilia,
Mbogholi
ni
Malaika,
wasoye
mauzauza.
Wasoye
mauzauza, wanasiasa asema,
Awaita
walooza,
kwa
makali
awachoma,
Kwamba
wanajidekeza, wote atakawatema,
Mbogholi
ni Malaika, ndiye aliyetimia.
Ndiye
aliyetimia, kama siasa ajua,
Nani
amemuambia, kina suluhu kifua,
Mpole
namuusia, pae kijuwa kutua,
Mbogholi
ni Malaika, kesho aende mbinguni.
Kesho
aende
mbinguni,
kusiko
hawa
majibwa,
Ajuwe
hayezekani, dunia iso na chapwa,
Siasa
daima duni, ni kunguru alorembwa,
Mbogholi
ni
Malaika,
Mpole
namshangaa!
SYLVESTER
OCHIENG
Almaarufu
“Kiroboto
Mpole”
Kituo
cha Lugha za Ughaibuni,
Eldoret.
No comments:
Post a Comment