Tuesday 17 July 2012

Mbogholi akoga

Mbogholi ni malaika?!

Mkwiro naukamata, kigoma nanzekipiga,
Mati natakaziita, zone Mbogoli kikoga,
Huyu mtoka Taveta, uungu akauiga,
Mbogholi ni Malaika, waja awona shetani.

Waja awona shetani, hasa wale wa siasa,
Amewatia doani, eti ni hakimu sasa,
Natakajua ni nani, Ludo amemtakasa,
Mbogholi ni Malaika, adharau viongozi.

Adharau viongozi, akawaita mikia,
Eti kikaza maozi, awaona masinia,
Naona akosa kazi, wengine kawangilia,
Mbogholi ni Malaika, wasoye mauzauza.

Wasoye mauzauza, wanasiasa asema,

Awaita walooza, kwa makali awachoma,

Kwamba wanajidekeza, wote atakawatema,
Mbogholi ni Malaika, ndiye aliyetimia.

Ndiye aliyetimia, kama siasa ajua,
Nani amemuambia, kina suluhu kifua,
Mpole namuusia, pae kijuwa kutua,
Mbogholi ni Malaika, kesho aende mbinguni.

Kesho aende mbinguni, kusiko hawa majibwa,
Ajuwe hayezekani, dunia iso na chapwa,
Siasa daima duni, ni kunguru alorembwa,
Mbogholi ni Malaika, Mpole namshangaa!

SYLVESTER OCHIENG
AlmaarufuKiroboto Mpole
Kituo cha Lugha za Ughaibuni,
Eldoret.

No comments:

Post a Comment