Mpole
nimeghasiwa, na waibaji wa miwa,
Nawamiminia
dawa,
sina
shaka
wauguwa,
Taksiri
niwatowa,
si
kwa
nia
kuumbuwa,
Wangu
ulie shambani, sondoke nao kiumbe.
Ungaingia
shambani,
una
uhuru
mwandani,
Chaguwa
pahala ndani, utapotulia chini,
Hata
kama mafichoni, sijali sitokuhini,
Wangu
ulie shambani, sondoke nao kiumbe.
Uubambue
maganda,
ubakiye
utakavyo,
Utende
utavyotenda,
upate
wako
mchovyo,
Kama
mcheza
kandanda,
shinda
jinsi
uwezavyo,
Wangu
ulie shambani, sondoke nao kiumbe.
Tafuna
kisha
unyonye,
utamu
saizi
yako,
Mie
nani
nikukanye,
shambani
sina
uchoko,
Maliza
chafu usanye, na uende uendako,
Wangu
ulie shambani, sondoke nao kiumbe.
Lakini
nakwonya wewe, mzoea kugurisha,
Ya
kwangu usiondowe, ukangia kuharisha,
La
sivyo nikuripuwe, kufisha nitakufisha,
Wangu
ulie shambani, sondoke nao kiumbe.
Kabula
nitie tuo, mwenye kono ujitenge,
Nikupa
langu
funguo,
na
mwako
pia
sifunge,
Nikija
nile chaguo, lolote usinipinge,
Wangu
ulie
shambani,
sondoke
nao
kiumbe.
Utunzi
wa: Malenga Kimpole,
Eldoret
(K).
Ni mas ala ya kuruhusu ukale
ReplyDelete