Saturday 4 May 2013

Kama kusoma mama


Nasema nao wadama, mawakili wa kusoma,
Wanaosema daima, kusoma ni kwa lazima,
Nipeni bila kukoma, sababu zinowatuma,
Kama kusoma ni mama, nambie baba ni nani?

Nambie baba ni nani, tena jina lake lipi,
Ndipo none tumaini, la sivyo sifa sikupi,
Bila kusoma jamani, wengi wanazila pipi,
Kama kusoma ni mama, nambie baba ni nani?

Mama huzaa hakika, akalea na kuasa,
Bali baba atakika, kunapojiri mikasa,
Basi wenzi nawataka, baba pewe ukurasa,
Kama kusaoma ni mama, nipe babna nifaulu.

Nipe baba nifaulu, kitabu sio mkate,
Nenda hata kwa hikalu, wahubiri nwakute,
Siketi nigeke mbulu, kamili wapi nipate,
Sawa kusoma ni mama, baba njoo unitunge. 


Malenga Sidi Kiroboto Mpole
Eldoret.

No comments:

Post a Comment